2014-01-14 08:14:51

Vatican na Cameroon watiliana sahihi mkataba wa ushirikiano


Serikali ya Cameroon, Jumatatu tarehe 13 Januari 2014 imetiliana sahihi mkataba na Vatican unaolitambua Kanisa Katoliki nchini Cameroon kisheria. Askofu mkuu Piero Pioppo, Balozi wa Vatican nchini Cameroon amoongoza ujumbe wa Vatican katika hafla hii na ujumbe wa Serikali ya Cameroon umeongozwa na Bwana Pierre Moukoko Mbondjo, Waziri wa Mambo ya nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Cameroon.

Mkataba huu una vipengele tisa vinavyobainisha nidhamu ya mahusiano kati ya Kanisa na Serikali ya Cameroon kwa kuhakikisha uhuru wa kila taasisi kwa ajili ya mafao na ustawi wa wananchi wa Cameroon: kimaadili, kiroho na kiutu. Uhusiano huu unapania kuchochea maendeleo ya mtu mzima: kiroho na kimwili, kwa pamoja wakitafuta mafao ya wengi.

Utekelezaji wa mkataba huu umeanza kazi baada ya pande mbili hizi kutiliana sahihi, kwenye Makao makuu ya Wizara ya mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Yaoundè, Cameroon.







All the contents on this site are copyrighted ©.