2014-01-13 09:50:31

Vatican na uhusiano wa kimataifa


Takwimu zinaonesha kwamba, kuna jumla ya nchi na mashirika ya kimataifa 180 yenye uhusiano wa kidiplomasia na Vatican. Tarehe 22 Februari 2013, Vatican ilianzisha uhusiano wa Kidplomasia na Sudan ya Kusini. Itakumbukwa kwamba, Vatican pia ina uhusiano wa Kidiplomasia na Umoja wa Ulaya, Shirika la Kitume la Malta na uhusiano wa pekee na Wananchi wa Palestina.

Vatican ina mwakilishi wa kudumu kwenye Umoja wa Mataifa na pia ni mwanachama wa kudumu katika Mashirika mengine 7 yaliyoko chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa. Vatican pia ni mtazamaji wa kudumu katika Mashirika 8 ya Kimataifa na Mashirikisho 5 ya Kikanda. Itakumbukwa kwamba, tarehe 5 Desemba 2011, Vatican ilikubaliwa kuwa ni Nchi wanachama wa Baraza la Kimataifa la Wahamiaji.







All the contents on this site are copyrighted ©.