Wakati huu Mama Kanisa anapokaribia kufunga Maadhimisho ya Sherehe za Noeli, yaani
kuzaliwa kwa Yesu Kristo Mkombozi wa ulimwengu kwa Sherehe za Ubatizo wa Bwana, Jumapili,
tarehe 12 Januari 2014, Baba Mtakatifu Francisko anawaalika kwa namna ya pekee, watumiaji
wa mitandao ya kijamii, kutafakari unyenyekevu wa Mwana Mpendwa wa Mungu, aliyezaliwa
katika hali ya umaskini.
Baba Mtakatifu anawaalika waamini na watu wote wenye
mapenzi mema kumuiga na kumwilisha fadhila hii kwa kuwamegea wengine, hasa maskini
na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa jamii, tone la upendo!