2014-01-10 15:21:58

imani thabiti ina uwezo wa kuayashinda malimwengu- Papa






Baba Mtakatifu Francisko, mapema Ijumaa hii aliwahakikishia waamini kwamba, imani thabiti ina uwezo wa kuyashinda malimwengu. Na ili wawena imani thabiti hadi kuyashinda ya kidunia, Wakristu, wanahitaji kuwa na ujasiri wa kumtegemea Mungu katika kila jambo. Lakini kwa bahati mbaya Kanisa limejaa wakristu wenye imani nusunusu, isiyokuwa na makali ya kuyashinda maovu ya kidunia. Papa Francisko alieleza katika mahubiri yake wakati akiongoza Ibada ya Misa mapema Asubuhi ya Ijumaa hii katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta hapa Vatican.

Kiini cha Mahubiri ya Papa , kiliangalisha katika barua ya kwanza ya Mtume Yohane ambamo anasisitiza ukweli wa maisha ya Kikristo kwamba ni kubaki katika Bwana, kumpenda Mungu na kumpenda jirani. Na kukaa ndani ya upendo huu wa Mungu ni utendaji wa Roho Mtakatifu, ambaye hutoa matunda thabiti ya imani.

Papa aliendelea kufundisha kwamba, yeyote anayekaa ndani ya Mungu, yeyote anayeumbwa na Mungu , na yeyote aishiye katika upendo wa Mungu huishinda dunia na ushindi huo ni imani. Alifafanua kwa upande wa Kimungu, ni kumkaribisha Roho Mtakatifu moyoni na kumwachia afanya kazi yake kwa neema zake. Na upande wa muumini ni kuwa na imani thabiti, ambayo ni ujasiri. Hiyo ndiyo nguvu inayomwenzesha muumini kuushinda ulimwengu. Kumbe Imani kwa Kristu inaweza kufanya kila kitu ! Imani ni ushindi !
Papa Francisko alieleza na kurudia kusisitiza , njinsi ilivyo vyema hata kwetu, kuuuishi msititizo huu, kutokana na ukweli kwamba, Wakristu wengi hushindwa kuuishi upendo wa Mungu, ambayo kiukweli ni majitolea ya bila kujibakiza kwa ajili ya wengine. Ameonya waamini wengi wa kanisa, huuishi upendo huu kinusunusu, na hivyo kwa kushindwa kutimiza yale yanayotakiwa katika kuwa mtu mkamilifu kiimani. Na hivyo wengi, huanguka katika mitengo ya mwovu na kutenda kinyume na tabia ya upendo Kristu, wakishindwa kukaa ndani ya Mungu, na kumezwa na Malimwengu. Kanisa limejaa Wakristu wa aina hii walioshindwa na malimwengu ambao hawaamini katika ushindi huu wa kukaa na Mungu, ushindi wa imani.Wasiokuwa na Upendo kwa Mungu na kwa jirani, hawako hai ndani ya imani na hivyo ni watu walioshindwa na mkuu wa dunia hii , Ibilisi.

Papa alieleza na kumsifu mwanamke Mkanaani na yule mtu aliyezaliwa kipofu , kwamba imani yao ilikuwa thabiti na hivyo kuwa na uwezo hata wa kuhamisha milima.

Papa pia ligusia suala la kuabudu kwa unyenyekevu akisema , akisema, iwapo tunajua jinsi ya kumwomba Mungu na jinsi ya kumshukuru pia tunapaswa kujua namna ya kumwabudu na kumtukuza. Na kwa mba kwa ufahamu wake wa maisha ya kanisa, waamini wengi si makini katika kuabudu au kutokana na ufahamu mdogo katika kuabudu, au kutojali na hivyo huiugama imani yao kijuujuu bila kuwa makini na uhakika.
Kwa muonohuo,Papa Francisko amesisitiza kwamba, kila Mkristu, anapaswa kujua namna ya kuabudu vyema na namna ya kuikiri imani na kuitunza, kama tabia sehemu ya tabia yake katika maisha ya kila siku.







All the contents on this site are copyrighted ©.