2014-01-08 15:51:54

Katekesi ya Papa kwa mahujaji na wageni


Baada ya Siku Kuu ya Noel, mwaka Mpya na Epifania, Jumatano hii, Baba Mtakatifu ameanza utoaji wa Katekesi zake za Jumatano kwa mahujaji na wageni.
Na aliifungua Katekezi ya kwanza na maelezo kwamba, kwa mfululizo atatoa katekesi juu ya Sakramenti ya Ubatizo, katika umuhimu wake, kama pia inavyotajwa katika Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican kwamba, Kanisa lenyewe ni " sakramenti ", ishara iliyojaa neema, ambayo hufanya kazi ya kuokoa ya Kristo, iendelee kuwepo hata sasa katika historia, kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
Alieleza na kuitaja Sakramenti ya Ubatizo kuwa ya kwanza katika sakramenti saba za Kanisa , ubatizo wenye kutuwezesha kuzaliwa upya katika Kristo, na kutufanya kuwa washiriki katika siri ya kifo chake na ufufuko wa Kristu, ukitupatia dhamana ya msamaha wa dhambi na kutuweka sisi upya huru, kama watoto wa Mungu na washarika wa Kanisa lake.
Papa alieleza na kuwasisitizia waamini wasisahau zawadi kubwa wanaoipata kwa kubatizwa. Ubatizo unaotubadili , na kutupa tumaini jipya kuu na kutuwezesha sisi kuingia katika upendo wa Mungu wa kukomboa watu wote, na hasa maskini , ambao wameivaa sura ya Kristo. Ubatizo wetu pia ametupa haki ya kushiriki katika kazi ya Kanisa za uinjilishaji , kama wanafunzi , na pia kama wamisionari.
Aliongeza, wakati huu tukisherehekea sikukuu ya Ubatizo wa Bwana Jumapili hii, sote na tumwombe Bwana awezeshe upya ndani mwetu kwa neema ya ubatizo wetu na pia kwa ndugu zetu wote na wake kwa waume , kuwa kweli watoto wa Mungu na washiriki hai wa Miwli wake ambalo ni Kanisa.
Baadaya yakatekesi Papa alisalimia katika lugha mbalimbali na kuwatakia furaha tele ya amani ya Bwana.








All the contents on this site are copyrighted ©.