2014-01-07 15:40:22

Papa afanya ziara fupi katika Parokia ya Mtakatifu Alfonso de Liguori - Roma


Jumatatu jioni, Papa Francisko alifanya ziara fupi katika Parokia ya Mtakatifu Alfonsi de ' Liguori ambako mamia ya watu, walikuwa wakimsubiri kwa hamu. Pamoja nae alikuwepo Vika wa Jimbo la Roma, Kardinali Agostino Vallini, Pia Askofu Guerino di Tora wa eneo la Kaskazini mwa JImbo la Roma.

Katika Parokia hiyo, Baba Mtakatifu alitembelea pango hai la Parokia hiyo ambalo lilionyesha hali halisi za wakati wa kuzaliwa Yesu kama ilivyoandaliwa na wanaparokia, kukiwa na wasanii mbalimbali wapatao 200 .

Baada ya kuwa na muda wa faragha katika sala na maombi ndani ya kanisa hilo, Papa Francisko alisalimia mstari mrefu wa waumini wapatao 200, walio wakilisha wanaparokia, mbele yao kukiwa na watoto na wagonjwa wa parokia hiyo.

Katika salaam zake za ujumla, Papa alisema, wanauanza mwaka mpya wakiwa na Yesu nae atabaki nao, kuwashindia maovu , na katika kuwafanya kuwa watu wa amani na sala . Pia Papa alitoa mwaliko kwa waamini kusali kwa ajili ya watu wote na zaidi sana kwa ajili ya watoto wanaozaliwa na kwa ajili ya wazee ambao ni hekima ya jamii.

Pamoja na watu wazima pia kuliandaliwa kundi la watoto wapatao mia waliomkaribisha Papa na wimbo maarufu “Wewe unayeshuka chini kutoka katika nyota”. Pia wakiwa na shada la kubwa la maua mekundu ya waridi.









All the contents on this site are copyrighted ©.