2014-01-06 10:11:17

Wananchi wanateseka Jamhuri ya Watu wa Afrika ya Kati!


Viongozi wa kidini Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa pamoja wametoa tamko kwa Jumuiya ya Kimataifa kuunganisha nguvu katika kuokoa maisha ya wananchi wengi wanaokabiliwa na hali ngumu kutokana na vita inayoendelea nchini humo. Inasikitisha kuona kwamba, vita hii imegeuzwa kuwa ni vita ya kidini, hali ambayo imepelekea wananchi wengi kuyakimbia makazi yao na hivyo kujikuta wanaishi katika makazi ya muda ambayo bado hayajaandaliwa vyema!

Askofu mkuu Dieudonnè Nzapalainga wa Jimbo kuu la Bangui na Shiekh Omar Kobine Layama, Imam mkuu wa Mji wa Bangui, kwa pamoja wanaomba Umoja wa Mataifa kupeleka vikosi vya kulinda amani Jamhuri ya Afrika ya Kati, ili kuokoa maisha ya maelfu ya watu ambayo kwa sasa yako hatarini. Mashirika ya Misaada ya Kanisa Katoliki yanaendelea kuwahudumia wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi mjiji Bangui.







All the contents on this site are copyrighted ©.