Washirikisheni wengine furaha inayobubujika kutokana na urafiki wenu na Yesu!
Katika pilika pilika za Maadhimisho ya Noeli na Mwaka Mpya 2014, vijana ambao kimsingi
ndio wadau wakuu katika mambo haya, Baba Mtakatifu Francisko anawakumbusha vijana
kwamba, Yesu anapenda kujenga na kuimarisha urafiki na kwamba, anawataka vijana kuwamegea
wengine furaha inayobubujika kutokana na urafiki huu.