Mheshimiwa Padre Fèlicien Mwanama Galumbulula ateuliwa kuwa Askofu mpya wa Jimbo la
Luiza, DRC
Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi lililowasilishwa kwake na Askofu Lèonard Kasanda
Lumembo, C.I.C.M wa Jimbo Katoliki la Luiza la kung'atuka kutoka madarakani kadiri
ya Sheria za Kanisa namba 401§ Ibara ya 1.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu
Francisko amemteua Mheshimiwa Padre Fèlicien Mwanama Galumbulula, Jaalim wa Chuo Kikuu
na Katibu Mwambata wa Baraza la Maaskofu Katoliki DRC kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki
la Luiza, DRC. Askofu mteule Fèlicien Mwanama Galumbulula alizaliwa tarehe 26 Oktoba
1960. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi akapadrishwa tarehe 9 Agosti 1987.
Tangu wakati huo amefanya utume katika nyadhifa mbali mbali ndani na nje ya
DRC. Hadi kuteuliwa kwake, alikuwa ni Katibu Mwambata wa Baraza la Maaskofu Katoliki
DRC.