Rais wa Italia "achonga" na Baba Mtakatifu kwa njia ya simu!
Rais Giorgio Napolitano wa Italia katika shamra shamra za Mwaka Mpya wa 2014 amempiga
simu na kufanya mazungumzo na Baba Mtakatifu Francisko. Wametakiana kheri na baraka
tele kwa Mwaka 2014, ili kwa pamoja waendelee kukabiliana na changamoto zinazoendelea
kujitokeza kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi wa Italia na Jumuiya ya Kimataifa
katika ujumla wake.
Rais Napolitano katika salam zake za Mwaka Mpya kwa wananchi
wa Italia, alimshukuru kwa namna ya pekee Baba Mtakatifu Francisko kwa changamoto
za maisha na utume wa Kanisa nchini Italia. Naye Baba Mtakatifu Francisko wakati wa
Sala ya Malaika wa Bwana, alimshukuru Rais Napolitano na wananchi wa Italia kwa ujumla
wao na kuwatakia kheri na baraka kwa Mwaka 2014.