Mwenyezi Mungu hakujifua kwa nguvu na vitisho bali katika hali ya unyenyekevu!
Katika Kipindi hiki cha Noeli, waamini na watu wenye mapenzi mema wanapoendelea kutafakari
Fumbo la Umwilisho, Baba Mtakatifu Francisko anawakumbusha watumiaji wa mitandao ya
kijamii kwamba, Mwenyezi Mungu hakujifunua kwa nguvu na uweza mkuu, bali katika hali
ya unyenyekevu na unyonge inayojionesha kwa Mtoto mchanga!