Askofu Emmanuel Obbo, A.J. ateuliwa kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Tororo, Uganda
Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi la kung'atuka kutoka madarakani lililowasilishwa
kwake na Askofu mkuu Denis Kiwanuka wa Jimbo kuu la Tororo, Uganda kadiri ya sheria
za Kanisa namba 401ยง Ibara ya 1.
Baba Mtakatifu amemteua Askofu Emmanuel Obbo
kutoka Shirika la Mitume wa Yesu, kuwa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Tororo. Kabla ya
uteuzi huu, Askofu mkuu mtarajiwa Emmanuel Obbo alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki
Soroti. Baba Mtakatifu amemteua pia kuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Katoliki la
Soroti.