".. Bwana akubarikie, na kukulinda. Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani.." (Hesabu 6:22-27).
Mwaka mpya
2014 umeanza. Tushukuru Mungu kama tuliuanza katika mazingira ya kanisani kwa Ibada
au hata kwa sala fupi na familia zetu. Kuna waliouanza, kwa bahati mbaya katika bar
au fukwe za bahari. Hujachelewa bado, fanya hima katika juma hili ufanye ibada fupi
na familia yako ili uanze na Mungu Baba.
Waisraeli walitamani sana kuanza kila
kitu kwa baraka. Na ndio maana Mungu alimpa Musa "formula" hii ya baraka ili kuzima
kiu yao. Tuone umuhimu wa baraka katika Maisha yetu. Tusikurukupe kwa cho chote Mwaka
huu. Tuwe na unyenyekevu wa kuomba baraka. Omba misa kanisani kwa lo lote unalonuia
kufanya. Usifanye kwa akili na karama yako tu. Ujue wazi, Bwana asipoujenga mji waujengao
wafanya kazi bure.
Tuombe :
Baba twaingojea kwa hamu sana kila Baraka
utakayotukirimia kwa Mwaka huu mpya 2014. Baba uwe faraja na kimbilio la kila mmoja
ndani ya familia zetu, kazi zetu, watoto wetu na rafiki zetu. Nyoosha mkono wako kwa
kila familia zetu.
Imeandaliwa na Padre Beno Michael Kikudo Jimbo kuu
la Dar es Salaam.