Sala ya Papa Francisko kwa Familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefu
Mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, katika Maadhimisho ya Sherehe ya Familia Takatifu
ya Yesu, Maria na Yosefu, Jumapili tarehe 29 Desemba 2013 akiwa kwenye Uwanja wa Kanisa
kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Baba Mtakatifu alisali sala maalum kwa ajili
ya kuombea familia duniani:
Yesu, Maria na Yosefu, ndani mwenu tunatafakari
mng’ao wa upendo wa kweli, tunawatumainia. Familia Takatifu ya Nazareti, zijalie familia
zetu pia ziwe ni mahali pa sala, shule makini ya Injili na Makanisa madogo ya nyumbani.
Familia Takatifu ya Nazareti, tunakuomba kusiwepo tena matumizi ya nguvu,
hali ya kujifunga na migawanyiko katika familia zetu; tunakuomba kwa ajili ya wale
waliojeruhiwa na kukwazika, waweze mapema iwezekanavyo kufarijika na kuponywa.
Familia
Takatifu ya Nazareti, tunakuomba kwa ajili ya Sinodi maalum ya Maaskofu, iamshe tena
dhamiri ya kila mmoja kuhusu utakatifu na tabia ya familia, uzuri wake kadiri ya mpango
wa Mungu. Yesu, Maria na Yosefu, sikiliza sala yetu na ututimizie. Amina.