Masifu ya Jioni kwa ajili ya Siku kuu ya Bikira Maria Mama wa Mungu
Baba Mtakatifu Francisko, Jumanne, tarehe 31 Desemba 2013 majira ya jioni, anatarajiwa
kuongoza Masifu ya jioni kwa ajili ya Maadhimisho ya Siku kuu ya Bikira Maria Mama
wa Mungu na kesha kwa ajili ya Siku ya 47 ya Kuombea Amani Duniani kwa Mwaka 2014,
inayoongozwa na kauli mbiu "udugu ni msingi na njia ya amani."
Mara tu baada
ya Masifu ya Jioni, kutafuatia Ibada ya Kuabudu Ekaristi Takatifu; Utenzi wa shukrani
kwa Mwenyezi Mungu, Te Deum na baadaye, Baraka kuu kwa kufunga Mwaka 2013. Kanisa
linamwelekea Yesu Kristo ili kumwabudu, kumshukuru na kumtukuza kwa wema na ukarimu
wake!
Linamkimbilia kuomba huruma na msamaha kutokana na mapungufu ya Watoto
wake waliotawanyika sehemu mbali mbali za dunia pamoja na kuomba baraka ya kuendelea
kuwa na imani na matumaini kwa siku za usoni.