Watoto mashahidi waliouwawa kikatili enzi ya Mfalme Herode
Mashahidi na wafiadini wanatoa ushuhuda kwa Kristo na Kanisa lake si tu kwa njia ya
maneno, bali kwa kuyamimina maisha yao. Wafiadini na mashahidi wanaendelea kulikumbusha
Kanisa kwamba, kifodini ni zawadi kubwa kutoka kwa Yesu Kristo mwenyewe. Tarehe 28
Desemba, kila mwaka, Mama Kanisa anawakumbuka watoto waliouwawa kikatili na Mfalme
Herode, alipokuwa anayawinda maisha ya Mtoto Yesu.
Watoto hawa ni kati ya
wale wanaomzunguka Mwanakondoo wa Mungu na kwa njia ya ushuhuda makini wa watoto hawa,
Mama Kanisa anapenda kukumbusha umuhimu wa kuthamini, kulinda na kutetea ut una heshima
ya watoto.
Baba Mtakatifu Francisko katika Waraka wake wa Injili ya Furaha
anabainisha kwamba, Uinjilishaji ni dhamana inayotekelezwa na Mama Kanisa kwa kufuata
amri ya Kristo, kwenda duniani kote ili kubatiza na kuwafundisha yote aliyo agiza.
Dhamana hii inatekelezwa na Familia yote ya Mungu katika ujumla wake.
Baba
Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI katika Waraka wake wa kichungaji, Dhamana ya Afrika
anasema kwamba, watoto ni zawadi ya Mungu kwa wanadamu, kumbe, wanapaswa kuwa ni lengo
la: Familia, Kanisa, Serikali na Jamii katika ujumla wake, kwani watoto ni chanzo
cha matumaini na maisha mapya. Mwenyezi Mungu yuko karibu na watoto na kwamba, wanathamani
kubwa sana mbele yake. Mtoto ana haki ya kuishi na kwamba, Kanisa Barani Afrika lazima
lisimame kidete kuwalinda na kuwatetea watoto tangu pale wanapotungwa mimba tumboni
mwa mama zao hadi mauti ya kawaida inapowafika.
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto
XVI anaendelea kusema kwamba, ni jukumu la Kanisa kuhakikisha kwamba, linaruhusu mwanga
wa Kristo ung’ae maisha ya watoto kwa kuwapatia upendo wake kwani kwa hakika wana
thamani kubwa sana mbele yake. Mwenyezi Mungu anataka kila mtoto awe na furaha na
tabasamu; na upendeleo wake uwe juu yao, kwani ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu
wanyenyekevu kama walivyo watoto.
Tarehe 28 Desemba ya kila Mwaka, Mama Kanisa
anafanya kumbu kumbu ya Watoto waliouwawa kikatiliki na Mfalme Herode alipokuwa anamtafuta
Mtoto Yesu aliyekuwa amesikia habari zake. Hii ni Siku ambayo Shirika la Utoto Mtakatifu
nchini Tanzania linafunga Mwaka wa Imani rasmi.
Padre Deusdedith Mulokozi,
C.PP.S anaangalia msingi wa Utoto Mtakatifu, Majukumu ya wazazi na lengo kuu la Chama
cha Utoto Mtakatifu. Hii inatokana na ukweli kwamba, Kanisa linaendelea kuwekeza katika
malezi na makuzi ya Watoto ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa Uinjilishaji
wa kina kwa watoto wenzao!
I MSINGI WA UTOTO MTAKATIFU
Ni utoto
mtakatifu wa Yesu Ni mwaliko wa Mkombozi wetu Yesu Kristo Waache watoto waje
kwangu kwa maana ufalme wa Mungu ni wao (Mt. 19:14) Anawaita wawe rafiki, wasaidizi
na wamisionari wake kwa yale mengi aliyowatendea Wanaitwa waishi ujumbe wanaoitwa
kuupeleka kwanza kabla ya kuupeleka kwa wengine\ujumbe huo ni Injili Takatifu yaani
habari njema kwetu sisi sote Yesu hana mikono, macho, mdomo, miguu au nguo ya kuvaa,
kwa sasa yeye ni maskini wa maskini, na hivyo anataka mtumie mikono, macho, midomo
na yote mliyo nayo kusaidia maskini Nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa
na kiu mkanipa maji, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkaja kunitazama, nilikuwa
gerezani mkaja kunitembelea (Mt. 25:34-37). Watoto wa Utoto Mtakatifu, wanaalikwa
kuwa watu wa IBADA, KUSHIRIKI SAKRAMENTI ZA KANISA NA HASA KITUBIO NA MISA TAKATIFU
II
MAJUKUMU YA WAZAZI
Wazazi tunzeni uhai, ninyi ndio wamisionari wa kwanza
tangu dakika ya uhai wa mwanadamu Mfunze mtoto namna ya kuishi vizuri naye hatasahau
njia hiyo hata uzeeni (Methali 22:6) Wazazi wawe alama ya furaha katika familia
na uhai wa kanisa Mwache Roho Mtakatifu afanye miujiza yake kwa ninyi kujifungua
mioyo yenu
III LENGO Watoto wasaidie watoto wenzao Kufikia lengo
hilo inawapasa wazazi, walezi, makatekista, walimu wa dini, watawa, mapadre kuwapa
malezi bora ya Imani Katoliki Kuwasaidia kujua utume wao Yesu anapenda watoto
waokolewe kutoka kila aina ya uovu kimwili na kiroho Kumtafutia Yesu marafiki wa
Imani yao na wasio wa imani yao.