2013-12-28 10:24:51

Wanajeshi 5,500 wa Umoja wa Mataifa wapelekwa kulinda raia na mali zao


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeamua kwa akuli moja kuongeza idadi ya wanajeshi wa kulinda amani nchini Sudan ya Kusini ambayo kwa sasa iko kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Taarifa ya Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon inaonesha kwamba, wanajeshi 5, 500 kutoka Umoja wa Mataifa wanapelekwa Sudan ya Kusini ili kuongeza nguvu katika mchakato wa kulinda raia na mali zao. Umoja wa Mataifa unasema kwamba, kuna zaidi ya watu laki moja moja ambao kwa sasa wanaishi kwenye Kambi maalum za wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi nchini Sudan ya Kusini.

Kuna idadi kubwa ya raia ambao wamepoteza maisha yao kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea Nchi Sudan. Hata hivyo juhudi za Jumuiya ya Kimataifa ya kutaka kupata suluhu ya amani na utulivu zinaendelea kufanyika ndani na nje ya Sudan ya Kusini. Wanachama wa IGAD chini ya Rais Yoweri Museveni wa Uganda wanafuatilia kwa karibu zaidi machafuko ya kisiasa nchini Sudan ya Kusini kwani athari zake ni kubwa pia hata kwa nchi majirani.







All the contents on this site are copyrighted ©.