Papa mstaafu Benedikto XVI apata chakula cha mchana na Baba Mtakatifu Francisko
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Ijumaa, tarehe 27 Desemba 2013 amemtembelea
Papa Francisko na kupata chakula cha pamoja kwenye Hosteli ya Mtakatifu Martha iliyoko
mjini Vatican.
Hivi karibuni, Baba Mtakatifu Francisko alimtembelea Papa mstaafu
Benedikto XVI ili kumtakia kheri na matashi mema ya Siku kuu ya Noeli na kutumia fursa
hii kumkaribisha kwa chakula cha mchana, kwenye Hosteli ya Mtakatifu Martha, iliyoko
mjini Vatican.
Makatibu muhtasi pamoja na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu
mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican alialikwa kushiriki
pamoja na Monsinyo Bryan Wells mratibu wa shughuli za mjini wa Vatican.