Mchakato wa kutafuta suluhu ya amani Sudan ya Kusini
Viongozi wa Serikali kutoka Kenya na Ethiopia, siku ya Alhamisi tarehe 26 Desemba
2013 wamewasili Juba, Sudan ya Kusini kama sehemu ya mchakato wa kutafuta suluhu ya
amani katika vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea nchini Sudan ya Kusini.
Wakiwa
nchini humo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Waziri mkuu wa Ethiopia Bwana Hailemariam
Desalegn wamekutana na kuzungumza na Rais Salva Kiir wa Sudan ya Kusini. Viongozi
wa Jumuiya ya Kimataifa wanawataka viongozi wa Sudan ya Kusini kusitisha vita na kuanza
majadiliano ya amani. Rais Salva Kiir katika ujumbe wake wa Noeli anasema, yuko tayari
kufanya majadiliano na wapinzani wake.