Wazee wa Kanisa wakutana kutakiana kheri na baraka za Noeli kwa Mwaka 2013
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu jioni alikwenda kumtembelea Papa mstaafu Benedikto
wa kumi na sita, ili kumpatia salam na matashi mema ya Siku kuu ya Noeli kwa Mwaka
2013. Papa mstaafu Benedikto XVI alimpokea kwa heshima na taadhima Baba Mtakatifu
Franciko kwenye lango la kuingilia kwenye Makazi yake mapya ya Monasteri ya Mater
Ecclesiae iliyoko mjini Vatican.
Kwa pamoja walikwenda kusali kwa kitambo kidogo
kwenye Kikanisa na kufuatia mazungumzo ya faragha yaliyodumu kwa kitambo cha dakika
thelathini. Baba Mtakatifu Francisko alipata pia fursa ya kusalimiana na "Familia"
ya Papa mstaafu Benedikto XVI.