2013-12-23 11:27:41

Kagera yahimizwa kudumisha umoja na mshikano -Askofu Msaidizi Kilaini


Askofu Msaidizi Methodius Kilaini wa Jimbo Katoliki la Bukoba, amehimiza wakazi wa Mkoa wa Kagera kuona umuhimu wa uvumilivu wa kidini, kwa ajili ya udumishaji amani na maelewano, kama ambavyo siku zote Watanzania wamekuwa wakiishi , kutokana na watanzania wengi kujenga roho bora imara, yenye uelewa mpana katika masuala ya kisiasa na kiutamaduni . Pia ametoa wito kwa wazazi kuhakikisha wanapata muda wa kutosha kutoa malezi kwa watoto wao, ili watoto waweze kupata majiundo sahihi katika kuwa raia wema.

Askofu Kilaini alitoa wito huo, Jumanne iliyopita, katika hotuba yake ya kumpongeza Askofu Mstaafu wa Jimbo la Bukoba , Askofu Nestorius Timanywa (76) , ambaye amestaafu baada ya kuliongoza Jimbo la Bukoba kwa miaka 39.Hotuba iliyonukuliwa na Allafrica.

Alisema wakati wanasherehekea tukio hilo, ni muhimu kuzichukua sherehe hizi kama somo la kujifunza kutoka Roho wa mstaafu, Askofu Timanywa, jinsi alivyoweza kuwaunganisha watu wa imani mbalimbali za kidini, wakati wote wa utawala wake . Na ndivyo inavyotupasa kushikilia na kutoruhusu kabisa dini kuwa kigezo za kuigawa jamii.

Mungu aliumba watu wote sawa . Na hivyo tunapaswa kuhakikisha kwamba, tofauti za kidini hazitutenganishi au kutugawa katika maisha ya kijamii ya kila siku.
Askofu Kilaini alieleza na kuongeza wakati uongozi wa Askofu Timanywa, mlizaliwa Maaskofu wengine watano waliowekwa wakfu. Aliwataja Askofu Damian Kyaruzi wa Jimbo la Sumbawanga, Askofu Msaidizi Methodius Kilaini wa Jimbo la Bukoba, Askofu Desiderius Rwoma wa Jimbo Bukoba , Askofu Almachius Rweyongeza wa Jimbo la Kayanga - Karagwe Na Askofu Mkuu Novatus Rugambwa wa Jimbo la Sao Tome na Principe.Na pia alitaja jinsi Askofu Timanywa alivyo shuhudia kuundwa kwa majimbo mapya matatu , Geita, Bunda na Kayanga - Karagwe.

Askofu Timanywa alizaliwa tarehe 7 Mei 1937 parokiani Mugana , wilayani Misenyi Kagera. Alipadrishwa Desemba 11 , 1966 , wakati Kardinali Laurian Rugambwa, alipohamishiwa Dar es Salaam kuwa Askofu Mkuu wake na Askofu Gervas Nkalanga alipofanywa kuwa Askofu wa Jimbo la Bukoba, hadi alipostaafu kutokana na hali ya afya , na Askofu Nestory Timanwa kuchaguliwa kuwa Askofu Februari 24, 1974. Mwaka 1992, Jimbo la Bukoba lilifanya sherehe ya kutimiza miaka mia tangu ukatoliki kuingia katika eneo hilo.








All the contents on this site are copyrighted ©.