Jengeni ukimya, ili kusikia sauti ya upendo wa Mungu ndani mwenu!
Mara nyingi Noeli imekuwa ni siku kuu ya pilika pilika za maisha, kiasi kwamba, watu
wanakosa utulivu na amani ya ndani. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa
watumiaji wa mitandao ya kijamii anawaalika kwa Noeli ya Mwaka huu, kuanza kujenga
utamaduni wa ukimya, ili kuweza kuisikia sauti ya upendo wa Mungu katika maisha ya
mwanadamu!