Wakati huu Mama Kanisa anapoendelea kufanya tafakari ya kina kuhusu Fumbo la Umwilisho,
tayari kushiriki katika Siku kuu ya Noeli ambayo inabisha hodi mlangoni, Baba Mtakatifu
Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anakumbusha kwamba,
kipindi cha Majilio ni hija ya maisha ya kiroho kuelekea Bethlehemu.
Anawaalika
kujiachilia mikononi mwa Mwenyezi Mungu ili waweze kuongozwa na Mwanga wa Mungu aliyefanyika
mwili!