Rais Jakaya Kikwete kukabidhiwa Rasimu ya Katiba Mpya ya Tanzania
Tume ya Mabadiliko ya Katiba inapenda kuwafahamisha wananchi na wadau wengine wote
kuwa Hafla ya kukabidhi Rasimu ya Katiba kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe. Dr. Ali Mohammed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi itafanyika siku ya Jumatatu, Desemba 30, 2013 katika Viwanja
vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo pia inatarajiwa kuhudhuriwa
na viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, taasisi za kidini, asasi za kiraia na wananchi
wa kawaida.