Kheri na Baraka Papa Francisko kwa kutimiza miaka 77 ya kuzaliwa kwako!
Baraza la Maaskofu Katoliki Italia limemtumia ujumbe wa matashi mema Baba Mtakatifu
Francisko anapoadhimisha kumbu kumbu ya kuzaliwa kwake. Wanamshukuru kwa kujitosa
bila ya kujibakiza kuwashirikisha watu Injili ya Furaha inayojikita katika maisha
na huruma ya Mungu, ili kufungua tena hija ya matumaini kwa wale waliokata tamaa!
Kanisa Katoliki nchini Italia linatambua na kuthamini mchango wake unaojionesha
kwa njia ya ushuhuda wa maisha. Waamini pamoja na wachungaji wao wanamsindikiza kwa
njia ya sala. Wanahidi kuendelea kutangaza Injili ya Furaha.
Wakati huo huo,
kituo cha Televisheni cha Vatican kimemtakia salam na matashi mema Baba Mtakatifu
Francisko kwa kuonesha picha maalum za matukio tangu alipochaguliwa kuliongoza Kanisa
Katoliki hadi alipoadhimisha siku yake ya kuzaliwa, akiwa amezungukwa na watoto wanaohudumiwa
kwenye Zahanati ya Mtakatifu Martha iliyoko mjini Vatican.