2013-12-17 10:35:31

Baa la njaa linanyanyasa watu zaidi ya millioni 2 nchini Afrika ya Kati!


Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa linasema kwamba, zaidi ya watu millioni mbili wanaoishi Jamhuri ya Watu wa Afrika ya kati wanakabiliwa na baa la njaa, ikiwa kama hatua madhubuti hazitachukuliwa na Jumuiya ya Kimataifa ili kunusuru maisha ya watu hawa!

Hii inatokana na uwepo wa vita na kinzani za kijamii kwa takribani mwaka mmoja zilizopelekea wananchi kujikuta wanayakimbia makazi na nchi yao. Inakadiriwa kwamba, kiasi cha asilimia 40 cha idadi ya watu wanaoishi vijijini wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, ikilinganishwa na wale wanaoishi mjini.

Wakulima wengi vijijini wanashindwa kutekeleza shughuli zao kwa kuhofia usalama wa maisha yao.







All the contents on this site are copyrighted ©.