2013-12-16 08:35:20

Tata Madiba amekamilisha safari ya maisha yake hapa duniani! Apumzike kwa Amani!


Wananchi wa Afrika ya Kusini wanaikumbuka sana Tanzania kutokana na mchango wake katika harakati za ukombozi kusini mwa Afrika, jambo ambalo limejenga urafiki na undugu wa dhati kati ya Afrika ya Kusini na Tanzania. RealAudioMP3

Tanzania chini ya uongozi wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilikuwa mstari wa mbele katika mapambono dhidi ya ukoloni na utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini kwa kuamini kwamba, binadamu wote ni sawa na Afrika ni moja.

Padre Dietrich Pendawazima, Makamu mkuu wa Shirika la Waconsolata, Jumapili tarehe 15 Desemba 2013 amewaongoza watanzania wanaosoma na kuishi mjini Roma kumkumbuka Tata Madiba aliyezikwa kwa heshima zote za kitaifa na kimila Kijijini kwake Qunu. Anasema, Mwalimu Nyerere alitamani sana kuona Bara la Afrika likiwa huru na kwamba, hii ndiyo ingekuwa furaha yake na chachu ya maendeleo endelevu kwa Bara la Afrika.

Tata Madiba amekamilisha safari ya maisha yake hapa duniani. Ni kiongozi ambaye ameacha urithi mkubwa kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi wa Afrika ya Kusini, Afrika na Dunia kwa ujumla. Watanzania pamoja na watu wote wenye mapenzi mema wanamhukuru Mungu kwa zawadi ya Tata Madiba na wanamwombea raha na mwanga wa milele! RIP. Amina.







All the contents on this site are copyrighted ©.