Monsinyo Georges Varkey Puthiyakulangara ateuliwa kuwa Askofu mwandamizi Jimbo Katoliki
la Port-Bergè, Madagascar
Baba Mtakatifu Francisko tarehe 15 Desemba 2013 amekubali ombi la kung'atuka kutoka
madarakani lililowasilishwa kwake na Askofu Armand Toasy wa Jimbo Katoliki la Port-
Bergè kadiri ya sheria za Kanisa namba 401§ 2.
Baba Mtakatifu amemteua Monsinyo
Georges Varkey Puthiyakulangara kuwa Askofu mwandamizi wa Jimbo hilo.