2013-12-14 11:36:00

Bwana Abdiweli Sheikh Ahmed ateuliwa kuwa Waziri mkuu mpya wa Somalia


Rais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia amemteua na kumtangaza Bwana Abdiweli Sheikh Ahmed kuwa Waziri mkuu mpya wa Somalia. Itakumbukwa kwamba, tarehe 2 Desemba 2013, Bunge la Somalia lilipiga kura ya kutokuwa na imani na aliyekuwa Waziri mkuu wa Somali Bwana Abdifarah Shirdon, aliyeondolewa madarakani kwa kura 250 dhidi ya kura 184 zilizotaka aendelee kubaki madarakani.

Wachunguzi wa masuala ya kisiasa wanasema, kura hii ya maoni inaweza kupelekea kuanguka kwa Serikali iliyoko madarakani. Baada ya Bunge kuridhia uteuzi wa Bwana Abdiweli Sheikh Ahmed ambaye kitaaluma ni mwanauchumi kuwa Waziri mkuu, atakuwa na siku 30 za kupanga tena upya Baraza la Mawaziri nchini Somalia.







All the contents on this site are copyrighted ©.