2013-12-12 10:57:31

Mali bado kunawaka moto!


Hali bado ni tete Kaskazini mwa Mali na matumaini ya hali ya amani kurejea tena katika siku za hivi karibuni yanaonekana kufifia baada ya mapigano makali kuzuka kati ya Jeshi la waasi na vikosi vya wanajeshi kutoka Ufaransa, vilivyoko nchini Mali ili kulinda amani na utulivu.

Mapigano haya yamepekea watu kadhaa kupoteza maisha yao na taarifa za kijeshi kutoka Ufaransa zinaonesha kwamba, Vikosi vya waasi vina uhusiano wa karibu na Kikundi cha Kigaidi, kilichojitwalia madaraka Kaskazini mwa Mali kunako mwaka 2012. Vikosi vya kijeshi kutoka Ufaransa vitaendelea kuwepo nchini Mali hadi hali ya amani na utulivu itakaporejea tena.

Juhudi za kulinda amani zinasimamiwa pia na vikosi vya kulinda amani kutoka Umoja wa Afrika. Bado kuna kinzani na migogoro ya kijamii nchini Mali, baada ya mapinduzi ya Serikali yaliyofanyika kunako mwaka 2012.







All the contents on this site are copyrighted ©.