2013-12-07 12:05:57

Mheshimiwa Padre Georges Bizimana ateuliwa kuwa Askofu mwandamizi wa Jimbo Katoliki Bubanza, Burundi


Baba Mtakatifu Francisko amemteua Mheshimiwa Padre Georges Bizimana kuwa Askofu mwandamizi wa Jimbo Katoliki la Bubanza, nchini Burundi. Askofu mwandamizi Bizimana ambaye kwa asili anatoka Jimbo Katoliki la Ngozi, hadi uteuzi wake, alikuwa ni Gombera wa Seminari kuu ya Jean Paul II, iliyoko Jimbo Katoliki la Gitega, Burundi.

Alizaliwa tarehe 12 Machi 1965, huko Buraniro, Jimbo Katoliki la Ngozi. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa tarehe 20 Agosti 1994. Baadaye akaendelea na masomo ya juu kuhusu taalimungu maadili mjini Roma. Tangu alipopadrishwa amewahi kuwa mlezi Seminarini, Paroko msaidizi Parokia ya Gasenyi, Paroko wa Parokia ya Mubuga na mkurugenzi wa miito.

Kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka 2008 alikuwa mjini Roma kwa ajili ya masomo, kwenye Chuo Kikuu cha Kipapa cha Alfonsiani. Mwaka 2008 hadi mwaka 2010 alikuwa ni Jalimu na kuanzia Mwaka 2010 hadi uteuzi wake alikuwa ni Gombera wa Seminari kuu ya Jena Paul II.







All the contents on this site are copyrighted ©.