Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri yake kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha,
kilichoko mjini Vatican siku ya Ijumaa, tarehe 6 Desemba 2013 amewataka waamini kujenga
moyo na bidii ya sala bila kuchoka wala kukata tamaa kama walivyofanya wale wakoma
wanaosimuliwa kwenye Injili, yule Mama mjane na Kipofu aliyepaza sauti yake hata Yesu
akaweza kumsikiliza na kumponya! Waamini waendelee kubisha hodi, iko siku Yesu atawasikiliza
na kuwatekelezea haja zao kadiri ya upendo wake.
Waamini wanaposali wawe na
imani thabiti na uhakika kwamba Mwenyezi Mungu ni mweza wa yote, wakimwomba anaweza
kuwatekelezea. Kama binadamu wanaelemewa pia na dhambi ambayo ni kikwazo katika ujenzi
wa uhusiano mwema na Mwenyezi Mungu; wawe na ujasiri wa kusema ukweli, ili watubu
na kumwongokea Mungu.