Vatican inaendelea kujizatiti katika mapambano dhidi ya utakatishaji wa fedha haramu
inayoweza kugharimia vitendo vya kigaidi!
Mamlaka ya Habari za Kifedha mjini Vatican, AIF, tarehe 4 Desemba, 2013 imetiliana
sahihi itifaki ya makubaliano na Mamlaka ya Habari za Kifedha nchini Ujerumani, BKA,
Itifaki hii imetiwa sahihi na Kardinali Attilio Nikora, Rais wa Mamlaka ya Habari
za Kifedha Vatican na kwa upande wa Ujerumani, Bwana Michael Dewald, Mkurugenzi wa
BKA ametia sahihi.
Lengo ni kuendelea kushirikiana katika ngazi ya kimataifa
katika mapambano dhidi ya utakatishaji wa fedha haramu inayoweza kutumiwa katika kugharimia
vitendo vya kigaidi sehemu mbali mbali za dunia.