Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Dokta Asha-Rose
Migiro, aluyekuwa Naibu Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwa Mbunge.
Taarifa
iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam, Jumanne, Desemba 3, 2013, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi,
Dokta. Florens Turuka inasema kuwa uteuzi huo umeanza Desemba 2, 2013. Dr. Asha-Rose
Migiro ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa
katika Chama cha Mapinduzi.