Juhudi za kukoleza mchakato wa majadiliano ya Kiekumene na Kanisa la Kiorthodox nchini
Romania
Kardinali Kurt Koch, Rais wa Baraza la Kipapa la Uhamasishaji wa Umoja wa Wakristo
pamoja na ujumbe wake, kuanzia tarehe 3 hadi tarehe 7 Desemba 2013 wako nchini Romania
kuangalia mwamko wa majadiliano ya kiekumene miongoni mwa Wakristo na kuanza mchakato
wa majadiliano na Kanisa la Kiorthodox nchini Romania.
Akiwa nchini humo,
Kardinali Koch na ujumbe wake, watapata fursa ya kukutana na kuzungumza na viongozi
wakuu wa Makanisa ya Mashariki pamoja na kukutana na viongozi wa Baraka la Maaskofu
Katoliki Romania. Ratiba inaonesha kwamba, Kardinali Koch amepangiwa pia kukutana
na viongozi wakuu wa Serikali nchini Romania.