2013-12-02 11:41:45

Nyenzo muhimu za Kipindi cha Majilio: Sala, tafakari na matendo ya huruma!


Waamini wanachangamotishwa na Mama Kanisa kujiandaa kwa Siku kuu ya Noeli kwa kujikita zaidi katika Sala, Tafakari ya Neno la Mungu, toba na wongofu wa ndani, kwani Noeli ni tukio linalomwezesha mwamini kukutana na Yesu Kristo Masiha.

Ni mwaliko uliotolewa na Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu, tarehe 2 Desemba 2013 wakati wa Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha kilichoko mjini Vatican. Noeli ni Siku kuu ya kukutana na Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai katika maisha ya imani, matendo mema na adili, mwaliko wa kumsikiliza Yesu kwa umakini mkubwa, ili kuonja furaha ya kukutana na Yesu katika hija ya maisha ya kila siku.

Baba Mtakatifu anawaalika waamini pia kutoa nafasi kwa Kristo ili aweze kukutana nao katika maisha yao ya kila siku, ili kuwaletea maisha mapya yanayosimikwa katika imani, matumaini na mapendo. Ili kuweza kukutana na Kristo kuna haja kwa mwamini kuacha moyo wake wazi, tayari kusikiliza na kutekeleza yale ambayo Kristo anataka kutoka kwa mfuasi wake. Waamini wanakumbushwa kwamba, Kristo anamsikiliza mmoja mmoja na wala si kama kundi la watu tu! Waamini wajitaabishe kukutana na kuonja upendo wa Kristo.

Hija kuelekea Siku kuu ya Noeli inawawezesha waamini kuwa wadumifu katika: tafakari, sala na matendo ya huruma ili kuwaonjesha maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii ile Injili ya Furaha








All the contents on this site are copyrighted ©.