2013-12-01 13:21:43

Papa awaasa Wanafunzi: niniyi ni watendaji na si watazamani-


Papa amewahimiza wanafunzi wa vyuo vikuu kutoathiriwa na maoni ya kilimwengu yanayo sababisha viwango vya maadili kummonyoko chini, lakini wadumishe moyo wa ujasiri wa kubaki aminifu katika Maadili ya Kikristu na kanuni za kidini. Kwa kufanya wataweza kupata nguvu na hekima za kusonga mbele na maisha adilifu, licha ya kupambana na mawimbi ya kilimwengu. Ni kudhamiria kutembea kwa imani na kuishi sambamba na Injili, inayo wasindikiza wakati wote huu wa kipindi cha majilio , na kuishi kwa uaminifu wa kiroho Siku Kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana , Noel.
Papa Francisko alitoa himizo hili Jumamosia, alipokutana na walimu na wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Roma ndani ya Kanisa la Mtakatifu Petro, akiendeleza utamaduni wa siku nyingi wa Papa kuadhimisha Ibada ya Sala ya Masifu kwa ajili ya kuzindua Jumapili ya kwanza ya majilio.
Papa Francisko akihutubia, alizungumzia Mungu kuingilia kati katika maisha ya muumini, kama ishara ya uaminifu wake. Alieleza , Mungu anapenda kuingilia kati kwa sababu anafahamu asili ya binadamu ni tete. Na Yeye ni aminifu kwa kazi yake aliyoianzisha kwa kila mmoja huumini , na daima huikamilisha. Na hili linampa muumini imani kubwa na uhakika wa usalama: imani kwamba anakaa ndani ya Mungu lakini Mungu anahitaji ushirikiano wa waamini kukubali kuongozwa nae na hasa katika utendaji wa maisha, na ushujaa wa kukabiliana na changamoto za nyakati hizi.
Papa aliendelea kuwaambia walimu na wanafunzi wa Vyuo Vikuu, kwamba mapenzi yao na uwezo wao ukiunganishwa na Roho Mtakatifu aliyekuja kukaa kati ya kila mmoja wao siku ya ubatizo , atawafanya kuwa watendaji na si watazamaji katika changamoto cha nyakati hizi.
Papa Francisko aliwatahadharisha wanafunzi kwamba, wameitwa kukabiliana na changamoto nyingi na nzito, kwa kuwa na nguvu ya ndani na ujasiri wa Injili. Na kwamba mazingira ya kijamii wanamoishi yanawalemea kutokana na kuzidiwa na udhaifu na mchoko wa upweke.
Papa amewatia moyo, akiwataka washinde changamoto hizo kwa kuyakabidhi maisha yao katika upendo wa Injili , usiomtupa mtu, na hivyo watasonga mbele na maisha ya kila siku bila kukata tamaa. Na amewataka wawe na ujasiri wa kubuni miradi mikubwa mpya lakini isiyo nyakua shauku yao kama vijana. Na itakuw ani makosa makubwa iwapo vijana watakubali kubaki wamefunga na fikra dhaifu za kufanana.

Ni kudhamiria kutembea kwa imani na kuishi sambamba na Injili, inayowasindikiza wakati wote huu wa majilio , na kuuiishi kwa uaminifu wa Roho wa Siku Kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana , Noel.
Mwisho wa Ibada hii, iliyohudhuriwa na mamia ya wanafunzi waliojaza ndani ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro hapa Vatican, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Brazil, walikabidhi Sanamu ya Bikira Maria, Kiti cha Hekima na Mlinzi wa wanafunzi kwa ujumbe wa Ufaransa.
Sanamu iliyochongwa na msanii mashuhuri Padre Marko Ivan Rupnik. Sanamu hiyo ilikuwa imekamilisha hija yake katikavyuo vikuu vya Brazil, ambako wanafunzi wamekuwa wakikusanyika na kutolea sala zao na kwa sasainaaendelea na hija hiyo, nchini Ufaransa







All the contents on this site are copyrighted ©.