Kwa ajili ya ujenzi wa umoja na mshikamano wa jamii nchini Italia, mjini Roma, tarehe
4 Desemba 2013, kutafanyika mkutano, utakao jumuiya wawakilishi wa dini mbalimbali,
za wahamiaji na watu mahalia wa Italia, wasomi , wanautamaduni, vyama na jumuiya
na taasisi mbalimbali za kijamii. Hii ni mara ya kwanza kwa mkutnao kama huo kufanyika
hapa Roma, na umeitishwa na Waziri wa ushirikiano wa kijamii nchini Italia , Waziri
Ce'Cile Kyenge. Lengo la mkutano ni wawakilishi kushirikishana maoni na fafanuzi
juu ya ukweli wa tunu za dini. Ni wakati wa kupanua mawazo na ufahamu juu ya imani
zingine , kwa ajii ya ujenzi wa amani, kuheshimiana na mshikamanowa jamii. Mratibu
Mkuu wa mkutano huu ni Yohane Roger, Mjumbe Maalum kutoka gazeti la Avvernire.
Kikao cha Tume ya Kimataifa Teologia Tume ya Kimataifa ya
Teolojia, inayoongozwa na Rais Askofu Gerhard Ludwig Müller,itakuwa na Kikao chake
cha mwaka Vatican 2-6 Desemba 2013. Kazi za Kikao hicho , zitafanyika chini ya usimamizi
wa Padre Serge Thomas Bonino , O.P. Katibu Mkuu.
Katika Kikao hiki , Tume
itaendelea kutafakari mada kuu tatu muhimu; suala la imani kwa Mungu mmoja. Pili maana
ya mafundisho ya kijamii ya Kanisa katika muono mpana wa mafundisho ya kikristo. Tatu
ni tatizo la Imani ya Kikristu kukubali. Mwishoni mwa kikao hiki, wajumbe wanatazamia
kukutana na Baba Mtakatifu Francisko.