Bwana Rolando Marranci ateuliwa kuwa Mkurugenzi mkuu wa Benki ya Vatican
Baraza kuu la Benki kuu ya Vatican limemchagua Bwana Rolando Marranci kuwa mkurugenzi
mkuu wa Benki ya Vatican, uteuzi huu unaanza rasmi tarehe 30 Novemba 2013.
Itakumbukwa
kwamba, kabla ya uteuzi huu, Bwana Marranci alikuwa ni mkurugenzi msaidizi wa Benki
ya Vatican; uteuzi uliokuwa umefanywa hapo tarehe 1 Julai 2013 na kuridhiwa na Baraza
kuu la Benki ya Vatican linaloundwa na Tume ya Makardinali.