2013-11-30 08:12:04

Akili ni zawadi ya Mungu


Mkristu huelekeza njia zake za mawazo kwa Mungu, na kukataa mawazo dhaifu yanayotaka kumweka mbali na Mungu. Ilikuwa kiini cha mahubiri ya Papa Francisko mapema Ijumaa, wakati wa Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta.
Papa alizungumzia juu ya mafundisho ya Yesu kwa wanafunzi wake juu ya kuzielewa dalili za nyakati akisema, Mkristu anapaswa kufikiri si kwa akili yake tu lakini kwa muono wa ndani wa moyo na kiroho. Na Mkristu, kufikiri kwa kuongozwa na Mungu ina maanisha , kukataa mawazo dhaifu yenye kuelekea katika kutenda dhambi.
Papa Francisko ameendelea kufundisha akirejea somo la Injili ambamo Bwana aliwafundisha wanafunzi wake kuzielewa dalili za nyakati , na ishara ambazo Mafarisayo hakuzifahamu. Amesema Wale ambao humfuata Yesu, si tu hufikiri kwa vichwa vyao, lakini pia kwa moyo na roho ndani, vinginevyo ni vigumu kuielewa njia ya Mungu katika historia.

Akirejea somo la Injili ya siku ambalo linazungumzia wanafunzi wawili wa Emmaus kukutana na Yesu, Papa alisema, si kwamba Yesu alikuwa na hasira kiasi hicho lakini alijifanya hivyo, wakati Wanafunzi wake waliposhindwa kuelewa mambo. Aliwaita wajinga, na wenye mioyo mizito , wasio elewa mambo ya Mungu na mwana wa mtu.
Papa anasema, hata kwetu leo hii, Bwana anatukemea kwa kutoelewa nini kinatokea katika maisha yetu, na hasa maisha binafsi , kile kinachotokea ndani ya moyo na kile kinachotokea katika ulimwengu , katika historia na kwa wakati huu. Papa ameziita hizi ni dalili za nyakati ! Kumbe , roho ya ulimwengu hutupa sisi mawazo mengine, kwa sababu roho wa ulimwengu hana mapenzi na watu, anapenda kuwaingiza wengi katika mtengo huu wa malimwengu wa bila kuwapa uhuru wa kuwaza vyema.

Roho wa ulimwengu, anayeshinikiza wote watembelee katika njia hiyo ya maovu , lakini kama alivyonya Mtume Paul, roho wa ulimwengu atatupeleka iwapo tu hatuna uwezo wa kufikiri juu yetu wenyewe, anaweza kutupeleka kasi,kama wasiokuwa huru.

Papa aliendelea kuzungumzia juu ya uhuru wa kufikiri akisema kwamba, ni kufikiri kwa uhuru, kwa lengo la kuelewa nini kinatokea. Lakini Binadamu peke yake hawezi. Anahitaji msaada wa Bwana. Tunahitaji kuelewa dalili za nyakati, na Roho Mtakatifu anatupa zawadi hii , zawadi ya akili ya kuelewa, si kwa sababu wengine wanasema nini kitatokea lakini ni uelewa wa ndani wa mtu mwenyewe.

Papa katika homilia hii, ametoa mwaliko kwa wote wanaotembea katika njia hii ya imani kujiuliza, Bwana anataka ni nini? Kuomba daima roho wa akili wa kuelewa dalili za nyakati. Kumwomba Yesu kwa neema hii, ili tupate na kumtumia roho wa akili, kukabiliana na mawazo dhaifu, yenye kuondoa ufahamu huu na kutuweka mbali na Mungu. Tuombe zawadi hii ya Roho wa akili katika kutafuta nini maana mambo na katika kuzielewa ishara za nyakati. Alihitimisha , tunaomba ni neema ya Bwana , tukiwa tumejawa na imani kwamba, Yeye ana uwezo wa kutupa Roho wa akili na kuelewa ishara za nyakati.








All the contents on this site are copyrighted ©.