2013-11-29 11:32:49

Wahamiaji kutoka Ethiopia wafukuwa Saud Arabia


Serikali ya Saud Arabia imewafukuza wahamiaji 40, 000 kutoka Ethiopia waliokuwa wanaishi nchini humo kinyume cha sheria tangu mapema Mwezi Novemba, 2013. Serikali imetoa vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini humo kwa wahamiaji millioni 4 kutoka sehemu mbali mbali za dunia.

Hayo yamebainishwa na Bi Dina Mufti, Balozi wa Ethiopia nchini Saud Arabia. Hadi kukamilika kwa zoezi hizi, zaidi ya wahamiaji 80, 000 watakuwa wamerudishwa nchini Ethiopia. Takwimu zinaonesha kwamba, sehemu kubwa ya wahamiaji hawa ni wanawake wanaofanyishwa kazi za nyumbani nchini Saud Arabia na wakati mwingi wanaishi katika mazingira hatarishi.

Taarifa za Serikali ya Ethiopia zinaonesha kwamba, Saud Arabia bado ina uhusiano mzuri na Ethiopia na kwamba, zoezi hizi halitaathiri uhusiano wa kidugu baina ya nchi hizi mbili.







All the contents on this site are copyrighted ©.