2013-11-29 11:19:06

Nyumba 185, 000 kujengwa kwa ajili ya wananchi wenye kipato cha chini


Rais Hifikepunye Lucas Pohamba wa Namibia ametangaza mpango mkakati wa ujenzi wa nyumba nafuu zipatazo 185,000 ili kuhakikisha kwamba, wananchi wa Namibia wanaishi katika makazi bora zaidi. Ujenzi huu unakwenda sanjari na huduma ya maji safi na salama pamoja na umeme.

Mkakati huu unawalenga zaidi wananchi wenye kipato cha chini Namibia ili hatimaye, kuondokana na makazi yasiyo rasmi yanayopaswa kubomolewa kwenye maeneo ya mijini nchini Namibia. Mpango huu unalenga kujenga wastani wa nyumba 12, 000 kila mwaka na unatarajiwa kukamilika ifikapo Mwaka 2030 kwa gharama ya billioni 4 na nusu za Marekani.







All the contents on this site are copyrighted ©.