Monsinyo Alfred Xuareb kusimamia mchakato wa mabadiliko Benki ya Vatican
Baba Mtakatifu amemteua Monsinyo Alfred Xuereb kuwa mwakilishi wake katika Tume ya
Kipapa inayohusika na Benki ya Vatican na Tume ya Kipapa ya Mabadiliko ya shughuli
za Benki ya Vatican na masuala yote ya uchumi wa Vatican.
Atakuwa na wajibu
wa kuangalia kwa ukaribu mwenendo wa tume hizi na kumpatia taarifa, kwa kushirikiana
na Sekretarieti ya Vatican kuhusu hatua muhimu ambazo atapaswa kuzichukua kama sehemu
ya utekelezaji wa majukumu yake.