Furaha ya Injili hujaa katika mioyo ya wanaokutana na kuishi na Yesu
Watu mbalimbali wanaendelea kutoa maoni yao juu ya Waraka wa Kwanza wa Kitume wa Papa
Francisko "Wenye jina: Furahi ya Injili (Evangelii Gaudium) ambamo ameanza na ujumbe
kwamba, Furaha ya Injili hujaa moyoni na katika maisha ya wale wanaokutana na Yesu.
Papa Francisko katika waraka huu anazungumzia mandhari ya kutangaza Injili
katika dunia ya leo na miongoni mwa mambo mengine, ameutazama kwa makini mchango wa
Sinodi ya Maaskofu iliofanyika hapa Vatican kwa Kaulimbiu : Uinjilishaji Mpya kwa
ajili ya kuieneza Imani, iliyofanyika Vatican, Oktoba 7 hadi 28 , 2012. Aidha wachambuzi,
mmoja wao akiwa Sergio Centofatti wanasema, pia Waraka huu ni muhimu kwa utume wa
Kanisa. Na unao nyesha mwelekeo wa njia ya Kanisa katika miaka ijayo.
Wachambuzi
hao wameyatenga yaliyoandikwa katika waraka huu wwenye kurasa 224, katika mafungu
matano ifuatavyo: 1.Uinjilishaji Mpya Waraka unalenga kuzindua
hatua mpya ya uinjilishaji wenye sifa ya kuwa na furaha katika kuinjlisha . Na ni
wito wa dhati kwa wakabatizwa wote, kuwa na mapenzi ya kuinjilisha, kwa sababu mapenzi
ya kufanya hivyo , yanatia nguvu katika kuwa na mabadiliko ya maisha yenye kuwavutia
wengine katika upendo wa Yesu, kama sehemu ya uzoefu wa maisha yao, furaha na uzuri
wa urafiki na Yesu , katika hali ya kudumu . Wakristo wameitwa kuwa wainjilishaji
kwa roho moja ya uchaji na utendaji , wa kutangazai Injili “kerygma " kwamba Yesu
Kristo anakupenda, alitoa maisha yake ili kuwaokoa, na sasa yu hai na yukio karibu
nawe kila siku, akikuangazia, kukupa ujasiri na kuweka huru dhidi ya dhambi. 2.Maadiliko
mapya, Ubunifu na umahiri Upya, ubunifu na umahiri , unaotokana na kurudia
kusoma upya Injili, ni sharti kwa Wachungaji na wale wote wanaofanya kazi za kitume
kwa ajili ya kufanya mabadiliko katika miundo, kwa kuwa katika kanisa, wote ni wamisionari
. Mabadiliko haya si Parokiani au majimboni tu lakini hata katika utawala wa kiti
cha Petro, kunahitajika uongofu mpya kwa ajili ya kutembea pamoja katika barbara ya
ushirikiano na mshikamano zaidi.Papa anasisitiza haja ya kuongeza jukumu kwa walei,
na kupanua uringo kwa ajili ya uwepo zaidi nafasi zaidi za utendaji wa wanawake katika
Kanisa, hasa katika maeneo ambapo wanawake huwa na nafasi ya kusikilizwa katika utoaji
wa maamuzi .
3.Kanisa lililo wazi, karimu na huruma. Waraka
wa Papa katika hili unalitaka kanisa kuwa wazi. Kanisa lililo tayari kumpoeka kila
mtu tena kwa moyo wa huruma na si kuhukumu, kwa sababu Mungu kamwe hachoki kusamehe.
Papa anahimiza waamini kutofungiwa milango ya Sakramenti, hata kwa sababu nyepesi.
Ameitaja Ekaristi kuwa si tuzo lakini ni ukarimu na chakula cha Bwana cha wanyonge
. Amewataka Wachugaji kutumia busara na ujasiri katika utendaji waowa kichungaji
ili kila mmoja ajisikie kupendwa na kanis alicha ya madhaifu yake. Na kwamba
kumtangaza Kristu kwa wale wasiokuwa na urafiki na Yesu, ni muhimu na lazima kuwa
na sifa chanya za ukarimu, heshima , huruma na uvumilivu bila ya kuchoka katika safari
hii ndefu nangumu. Katika hili Papa pia ametaja mahubiri ya mapadre ni lazima yaonyesha
neema hii ya matumiani ya yasiyo kuw ana ukomo, kutolewa daima kwa unyenyekevu na
huruma lakini kwa maneno yenye kupenya mioyo.
4Mahusiano ya karibu
kupitia njia ya kukutana na kujadiliana. Na Majadiliano na kukutana na
Wakristu wengine (Uekumene ), ni njia muhimu ya uinjilishaji, kama ilivyo pia katika
kukutana na dini zingine na wasio amani. HIli pia ni sharti muhimu kwa Mkatoliki
katika kueneza imani na amani. Mazungumzo ni lazima yafanyike katika hali ya uwazi
na furaha isiyokuwa na uficho katika uinjilishaji. Hasa, Papa alibainisha kuwa "
katika hili umuhimu utolewa zaidi katika kujenga mahusiano na waamini Waislamu. Papa
Francisko ameombahili lifanyike kwa unyenyekevu na uvumilivu wote, hasa katika mataifa
ya mapokeo ya Kiislamu kwa ajili ya kurejesha dhamana uhuru wa dini kwa Wakristo,
kama waumini wa Kiislamu wanavyo furahia uhuru huo katika nchi za Magharibi.
5.
Kanisa daima sauti ya kinabii. Kanisa ni sauti ya kinabii, yenye kuwa na
uwezo wa kusema kwa sauti ya ujasiri... hata dhidi mwelekeo pinzani wa kijamii.
Papa amelitangaza Kanisa, kuw ani Kanis aMaskini ka ajili ya Maskini. Hivyo Papa ametoa
wito kwa Kanisa maskini kuwa huduma ya maskini. Papa anakemea mifumo ya sasa ya kiuchumi
kwamba, haki imefunikwa na utendaji wa mimi kwanza. Na amerejea hali za maisha ya
watu masikini waliotupwa pembezopni na jamii na watoto ambao hawajazaliwa , na asili
ya muundo wa familia ya binadamu kuvurugwa, mateso na madhulumu kwa makundi manyonge
ya watu, akisema Kanisa linaakiwa kuwa mstari wa mbele kuwatetea wote hao.