2013-11-27 15:35:08

Bado kuna nafasi ya Amani- Libya


Pamoja na mvutano mkubwa wa kisiasa , Mons. Martinelli bado anaaamini uwepo wa mwanya wa amani-Libya

Shinikizo kali linaloendelea kwa ajili ya kufanikisha maridhiano ya kijamii, kwa hakika ni jambo jema, na lenye kuleta tumaini kwa Libya kuweza kupata tena hali ya utulivu na amani wakati wowote. Ni maelezo ya Askofu Mkuu Giovanni Innocenzo Martinelli , Mwakilishi wa Kitume, Tripoli , Libya, wakati akizungumza na shirika la habari la Fides.

AskofuMkuu Martinelli anasema, iwe katika mji wa Benghazi au kwa Tripoli kuna shinikizo kubwa kwa sababu makundi mbalimbali ya wanamgambo wanaofanya udhibiti katika miji hiyo miwili , wameanza kuweka silaha chini na kuruhusu vikosi vya usalama vya serikali kufanya shughuli zake.

Na kwamba Maandamano ya Novemba 15, karibu na makao makuu ya Tripoli yaliyofanywa na wanamgambo kutoka Misrata, yalichochewa na ufyatuaji wa risasi na kusababisha vifo 46 na zaidi ya 500 kujeruhiwa. Baada ya hilo, wakazi wa jiji hilo waliingia mitaani kuonyesha uvumilivu wao kwa uwepo wa makundi ya watu wa kawaida wenye kuwa na silaha. Hata katika Benghazi baada ya mapigano ya Jumapili , kati ya jeshi na wanamgambo wa Kiislam, yaliyo sababisha vifo 9 na 51 kujeruhiwa, Mamlaka ya mji huo Jumatatu, yaliruhusu maandamano ya amani mitaani kupinga hilo.

Na kwamba maisha katika jiji la Tripoli, sasa yako katika kipeo cha juu cha mivutano pia kama ilivyo katika mji wa Beghazi ambapo amebaki Mwakilishi w Kitume Mons Magro, na baadhi ya wafanyakazi wachache katika taasisi za kikanisa ameeleza Mons. Martinelli .
Akireje ahali hiyo anasmea kwa wakati huu , kanisa haliwezi kufanya mengi kuhusu kazi za kitume na kichungaji kwa jumuiya ndogo Katoliki, ambayo nayo inazidi kupungua siku hadi siku , na hasa baada ya Masista kuondoka kwa hofu za kushambulliwa na hivyo wamebaki wauguzi wachache ambao wanaendelea kutoa msaada na huduma ya thamani, katika hospitalini.
Mons. Martinelli amekiri kwamba, wanaunaishi wakati mgumu na wenye uchungu. Ni kitendawili cha Libya kinachohitaji kufumbuliwa , na bado kuna tumaini kwamba Walibya ipo siku wataweza kupatana na kuishi kwa amani.








All the contents on this site are copyrighted ©.