Wafadhili wasitisha misaada kwa Malawi kutokana na rushwa na ufisadi!
Serikali ya Malawi imepinga vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa na Umoja wa Ulaya, Uingereza,
Norway pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika, kwa kushindwa kusimama kidete kupambana
na rushwa, ufisadi pamoja na ubadhirifu wa mali ya umma nchini Malawi.
Bwana
Brown Mpinganjira, Waziri wa habari anasema, anashindwa kuelewa lengo la vikwazo hivi
kutoka katika Jumuiya ya Kimataifa kwa kusitisha kutoa misaada ambayo ni muhimu sana
kwa maendeleo ya wananchi wa Malawi!