Rais wa Paraguay akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 25 Novemba 2013 amekutana na kuzungumza
na Rais Horacio Manuel Cartes Jara kutoka Jamhuri ya Watu wa Paraguay, ambaye pia
amekutana na viongozi waandamizi kutoka Vatican chini ya Askofu mkuu Pietro Parolin,
Katibu mkuu wa Vatican.
Katika mazungumzo yao, viongozi hao wamepongeza uhusiano
mzuri uliopo kati ya nchi hizi mbili. Baadaye amejadili kwa kina na mapana kuhusu
hali halisi ya maisha ya wananchi wa Paraguay na Amerika ya Kusini katika ujumla wake;
mapambano dhidi ya umaskini, rushwa na ufisadi pamoja na mikakati inayopania kumwendeleza
mtu mzima: kiroho na kimwili sanjari na haki msingi za binadamu! Wamejadili pia mchango
wa Kanisa katika ustawi na maendeleo ya wananchi wa Paraguay. Kwa pamoja wameonesha
utashi wa nchi hizi mbili kushirikiana zaidi katika ngazi ya kimataifa.