2013-11-25 15:41:58

Kukamilika kwa mwaka wa Imani, ni mwaliko wa majitoleo zaidi katika imani,
maoni ya Salvatore Martinez.


Mwaka wa Imani uliozinduliwa na Papa Mstaafu Bendikto XV1, Octoba 2012 na kuhitimishwa na Papa Francisko, Jumapili 24 Novemba, umekuwa wa kipekee uliojaa lafudhi na utendaji mbalimbali wa kanisa katika umoja wa imani, ulioweka ujumbe wa Injili, kuwa kiini cha utendaji wote wa kanisa. Ni Maoni ya Rais wa Kitaifa wa Uhuisho wa Kiroho hapa Italy , Bwana Salvatore Martinez, akiutafakari mwaka wa Imani.
Katika mahojiano na Mwanahabari Federico Pianni, Martinez amekitaja kipindi cha mwaka mzima wa imani kwamba, kimekuwa ni kipindi kilicho leta mwamko kwa wengi kutazama hali halisi za imani katika maisha ya wengi. Wengi wanakubali kwamba imani imedhoofika kwa waaamini wengi. Wengi wamebaki katika hali ya uvuguvugu. Na hali hiyo inaleta haja ya kutamfuta mbinu mpya za kuimarisha imani , kutoa ufahamu zaidi kwa njia mbalimbali, ikiwemo kusoma na kutafakari upya imani, na historia ya Neno la Mungu kumwilishwa. Kuona kwa jinsi gani mtu bado anaweza kukombolewa na Injili na Kanisa kuumwilishi upendo wa Injili katika utendaji wake wote wa ubinadamu.
Na hivyo, Martinez anaendelea kusema, Papa Benedikto XVI, aliona haja ya kuweka katika kalenda ya Kanisa mwaka wa Imani, kama juhudi za kuufufua upya, yaliyo azimiwa na Kanisa katika maadhimisho ya mwaka Mtakatifu 2000. Na kujiuzuru ghafla Papa Benedikto katika utume wa kuliongoza Kanisa kama Papa, baada ya kuutangaza mwaka wa imani , kwa wengi kumetoa fundisho kubwa, hasa kwa waamini kusikiliza na kutenda kwa kadri sauti ya ndani inavyosema. Maamuzi ya kustaafu Papa Benedikto XV1, yameonekana kuwa kweli si maamuzi yake binafsi bali yalitoka kwa Roho Mtakatifu ambaye ni yuleyule aliyemweka katika nafasi yake Papa Francisko, anayeendelea kuonyesha ishara ya ukuu wa Papa duniani, kwa ajili ya Injili, na Kanisa la ulimwengu. Kanisa ambalo daima liko karibu na watu. Ukaribu unaotoa uelewa mpya zaidi wa maana ya Kanisa , kuwa ni upendo kwa watu wote. Ni upendo wa kmajitoleo ya kujibakiza na kuwa sadaka kwa ajili ya wengine.

Salvatore Martinez, alieleza huku akiangalisha pia katika malengo ya Kanisa baada ya mwaka wa imani, kama ilivyo ainishwa na Papa kwamba, lengo la kwanza kuendelea kuitangaza Imani kwa nguvu pande zote,za dunia bila kupunguza kitu , na kufanya uzuri wote wa Injili na ukweli wake uonekane kwa watu wote kama ilivyoandikwa katika waraka wa Lumen Fidei ... Lengo la pili ni waamini kuendelea kuihuisha upya imani, katika nyakati hizi za mabadiliko ya mifumo mipya ya maisha yanayo lenga kudhoofisha imani. Ni kuihuisha upya imani, kujikabidhi kwa Bwana wa Injili, kama tunayemkiri katika imani.
Lengo la tatu ni kutafuta jinsi watu wanavyoweza kurudisha imani yao kwa Kanisa. Kusema ndiyo kwa Kanisa, kwa sababu kwa wakati huu watu wengi wanaonyesha kuwa na imani kwa Yesu, lakini hawana imani na kanisa. Mwaka wa Imani imekuwa ni kipindi cha kusema ndiyo kwa Kanisa. Na hiyo ina maana ya kutambua kwamba, imani hii ni msingi wake umo katika mwili wa kanisa.
Pamoja na malengo hayo, kuna changamoto zilizo ainishwa Papa Francisko. . Kwanza ni jinsi ya kuleta mabadiliko mapya katika mifumo ya utendaji wa Kanisa na taasisi zake . Pili ni jinsi ya kufanikisha Uinjilishaji mpya, katika maana ya kuwa na uwazi zaidi kulingana na mahitaji ya nyakati zetu, dhamira kubwa kwa watendaji wa kanisa hasa wachungaji, ma wanapo fanya kazi ndani ya Kanisa, na pia kwa kila muumini, matendo yao yaweze kuushuhudia upendo wa Injili. Aidha kuna changamoto kwa viongozi kuwaongoza watu kwa upendo wa kina na huruma. Upendo na huruma, wakiiona kuwa ni kuwa ni zawadi ya imani itokayo kwa Mungu yenye kushukia kila muumini. Na hivyo, changamoto hii ni kwa kila Padre kigangoni parokiani na kusambaa hadi kitaifa na kimataifa.









All the contents on this site are copyrighted ©.