2013-11-22 15:21:14

Tunu msingi za mchezo wa rugby ziwawezeshe wanamichezo kufikia lengo kuu la maisha!


Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013 amekutana na kuzungumza na wachezaji wa timu za rugby kutoka Italia na Argentina. Amewashukuru na kuwapongeza kwa moyo wa urafiki unaojionesha baina ya mataifa haya mawili katika michezo ambayo wakati mwingine inalenga kusaidia kugharimia matendo ya huruma.

Baba Mtakatifu anasema rugby ni mchezo wa kupimana nguvu, unaohitaji kuheshimiana sanjari na kudhibiti tabia ya mtu binafsi na utashi kwani hapa "si maji kwa glasi kani yataka moyo kweli kweli" Ni mchezo unaopania kufikia lengo, kwani hata maisha ni mapambano yenye malengo, yanayohitaji moyo wa ushirikiano na mshikamano, kwa kusaidiana, ili kwa pamoja wote waweze kusherehekea ushindi.

Baba Mtakatifu anasema, si mtaalam sana wa mchezo wa rugby, lakini kama Askofu anauangalia mchezo huu kwa jicho la Kiinjili na kuwataka kuhakikisha kwamba, tunu msingi wanazozitumia katika mchezo wa rugby wanazitumia pia katika hija ya maisha yao nje ya uwanja wa rugby.







All the contents on this site are copyrighted ©.