2013-11-20 08:45:26

msikubali kuishi katika uchumba sugu!


Askofu msaidizi Eusebius Nzigilwa, Mwenyekiti wa Idara ya Katekesi, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano na Radio Vatican kama sehemu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani anabainisha kwamba, Sakramenti za Kanisa zinagusa hatua zote na nyakati zote muhimu za maisha ya Mkristo. RealAudioMP3

Zinayajalia maisha ya ya imani ya Mkristo, kuzaliwa na kukua, kupona na utume. Sakramenti ya Ekaristi takatifu ni "Sakramenti ya Sakramenti" inayopaswa kupokelewa na waamini waliojiandaa kukutana na Yesu Kristo katika hija ya maisha yao, tayari kwenda kumtangaza na kumshuhudia kwa njia ya maisha adili. Waamini wajitahidi kufanya maandalizi makini kabla ya kupokea Sakramenti za Kanisa huku wakiwa na moyo safi. Wasikubali kuishi uchumba sugu!

Askofu msaidizi Nzigilwa anawataka waamini kuhakikisha kwamba, wanajitahidi kuishi maisha adili kwa kuongozwa na amri za Mungu. Watambue kwamba, sheria ya Mungu imekwisha andikwa katika dhamiri zao, hivyo wanawajibika kulea na kuikuza dhamiri nyofu ili hatimaye, waweze kutoa maamuzi sahii ya kimaadili, kwa kutenda mema na kuachana na ubaya. Amri za Mungu ziwe ni dira na mwongozo wa maisha adili.







All the contents on this site are copyrighted ©.